Wananchi wanaendelea kumiminika kwa wingi katika Viwanja vya Maonesho vya Mwalimu Julius K. Nyerere, maarufu Sabasaba, kushuhudia Maonesho ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Maonesho hayo yameendelea kuvutia maelfu ya wageni wanaofika kujionea bidhaa, huduma, teknolojia na fursa mbalimbali za biashara kutoka ndani na nje ya Tanzania.




