Bila Uruma Mke Amkata Mumewe Uume na Kutupa Chini ya Kitanda Usiku wa Manane: Baraka Melami Alazwa Selian.

Geofrey Stephen
1 Min Read

Na Mwandishi wa A24tv.

Tukio Latikisa Olevolosi, Arumeru

Kijiji cha Olevolosi katika kata ya Kimnyaki, wilayani Arumeru mkoani Arusha kimeingia katika taharuki kufuatia tukio la kusikitisha ambapo mwanaume mmoja, Baraka Melami (40), amekatwa uume na mkewe, Anna Melami (30), usiku wa kuamkia Januari 19 majira ya saa saba usiku.

Habari Picha 4472

Maelezo ya Korosho la Tukio

Akiwa amelazwa katika Hospitali ya Selian Ngaramtoni, Baraka ameeleza kuwa mkewe alimsogelea kitandani kana kwamba alikuwa anajiandaa kwa tendo la ndoa. Lakini wakati Baraka akianza kupata hisia, Anna alichomoa kisu na kumkata sehemu zake za siri kisha kutupa kipande hicho chini ya uvungu wa kitanda.

Baraka anasema mkewe aliongeza sauti ya redio kwa makusudi ili kuficha makelele yake, jambo lililochelewesha msaada wa majirani. Ni baada ya kutoka nje huku akivuja damu ndipo alipoweza kupiga kelele na kusaidiwa.

Uongozi Watia Neno

Mwenyekiti wa kitongoji cha Juhudi, Jonas Kisite, amethibitisha tukio hilo akisema alipokea taarifa kutoka kwa majirani usiku huo na kuwatembelea ili kujionea hali halisi.

Aomba Msaada wa Matibabu

Baraka, ambaye kwa sasa anaendelea kupatiwa matibabu, ameomba watanzania wenye moyo wa huruma kumsaidia gharama za matibabu kutokana na hali yake kuendelea kuwa ngumu.

Mwisho.

Share This Article
Leave a Comment