PETS AFRICA WANG’ARA NANE NANE KWA KUONYESHA MBWA WA VIWANGO VYA KIMATAIFA.

Geofrey Steven
3 Min Read

Maonyesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nane  Nane. Jijini Arusha  yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuonyesha ubunifu katika sekta ya kilimo na mifugo. Mwaka huu, mmoja wa vivutio vikubwa katika viwanja vya maonyesho ni banda la Pets Africa, ambalo limevutia mamia ya wageni waliotaka kujionea mbwa wa pure breed wenye viwango vya kimataifa.

Habari Picha 19806

Katika banda hilo, wageni walipata fursa ya kuwaona mbwa wa aina ya Caucasian Shepherd na Alabai, wanaojulikana duniani kwa uwezo wao mkubwa wa ulinzi wa mifugo na mali. Mbali na hao, kulikuwa pia na mbwa wanaofaa kwa familia kama Golden Retriever, Japanese Spitz na Maltese, ambao ni marafiki wazuri wa watoto na hufaa kufugwa nyumbani.
Akizungumza wakati wa maonyesho,

Habari Picha 19805

mwakilishi wa Pets Africa, Tanveer Hajee pamoja na  Adam, alisema lengo la kampuni hiyo ni kuongeza uelewa kuhusu ufugaji wa mbwa wa pure breed na kuchangia kuboresha ubora wa mbegu za mbwa nchini.

“Tumeleta mbegu bora kutoka nje ya nchi ili kusaidia kuboresha ufugaji wa mbwa Tanzania. Pia tunatoa elimu kuhusu namna ya kuchagua mbwa kulingana na matumizi yake, iwe ni kwa ulinzi au kwa familia,” alisema Tanveer.

Kwa mujibu wake, mbwa wa aina ya Caucasian Shepherd na Alabai wana silika za asili za ulinzi, jambo linalowafanya kuwa walinzi hodari hata kabla ya kupewa mafunzo rasmi.

Habari Picha 19808
Habari Picha 19807

Njiwa wa Urembo Wazidi Kuvutia Wafugaji.

Mbali na mbwa, wageni wengi walivutiwa pia na banda la mfugaji wa njiwa Adamu Abdu, ambaye amekuwa akifuga njiwa kwa zaidi ya miaka sita.

Adamu alionyesha aina mbalimbali za njiwa wa pure breed kutoka nchi tofauti, zikiwemo Chinese, Indian na American, ambazo zinajulikana kwa muonekano wao wa kipekee na hutumika zaidi kwa mapambo kuliko kwa matumizi ya chakula.

“Njiwa hawa ni wa urembo. Watu huwafuga ili kupendezesha mazingira ya nyumbani, lakini pia ni fursa nzuri ya biashara kwa wafugaji,” alisema.

Bei za njiwa hao huuzwa kwa jozi na zinaanzia Sh80,000 hadi Sh350,000, kulingana na aina ya breed.

 

Habari Picha 19811

Ufugaji wa Kisasa Unaendelea Kukua.

Ushiriki wa Pets Africa pamoja na wafugaji wa njiwa katika Maonyesho ya Nane Nane unaonyesha jinsi sekta ya ufugaji wa wanyama wa mapambo na wa ulinzi inavyoendelea kukua nchini.

Mbali na kuonyesha wanyama hao, washiriki walitumia maonyesho hayo kutoa elimu kuhusu ufugaji wa kisasa, umuhimu wa kutumia mbegu bora na namna shughuli hiyo inaweza kuwa chanzo cha ajira na kipato.

 

Habari Picha 19813

 

Habari Picha 19814

Kwa wanaotembelea Maonyesho ya Nane Nane, mabanda haya ni sehemu nzuri ya kujifunza zaidi kuhusu ulimwengu wa ufugaji wa mbwa na njiwa wa pure breed, huku wakipata fursa ya kuzungumza moja kwa moja na wataalamu wa sekta hiyo.

Mwisho .

Share This Article
Leave a Comment