DODOMA, Agosti 11, 2026 — Na Mwandishi wa A24tv .
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza S. Johari, amewasilisha maelezo ya Serikali kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 2 wa Mwaka 2026 (The Written Laws (Miscellaneous Amendments) (No. 2) Bill, 2026) mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria.
Mhe. Johari amewasilisha maelezo hayo leo, Agosti 11, 2026, katika shughuli za Bunge jijini Dodoma, ambapo Kamati hiyo imepokea na kujadili maelezo ya Serikali kuhusu muswada huo.

Muswada huo unapendekeza kufanya marekebisho katika sheria mbalimbali kwa lengo la kuboresha na kuimarisha utekelezaji wa sheria husika.
Miongoni mwa sheria zinazopendekezwa kufanyiwa marekebisho ni:

Sheria ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi, Sura ya 166;
Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya), Sura ya 287;
Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), Sura ya 288;
Sheria ya Baraza la Usalama la Taifa, Sura ya 61;

Sheria ya Uthamini na Usajili wa Wathamini, Sura ya 138; na
Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori, Sura ya 283.
Kwa mujibu wa maelezo yaliyowasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, marekebisho hayo yanalenga kuweka maboresho katika sheria hizo ili kuendana na mahitaji ya sasa ya kiutawala, kisheria na utekelezaji wa majukumu ya Serikali.


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, inayoongozwa na Mwenyekiti Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), imepokea na kujadili maelezo ya Serikali kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 2 wa Mwaka 2026.

Hatua hiyo ni sehemu ya mchakato wa Bunge wa kuchambua na kujadili miswada ya sheria kabla ya hatua zinazofuata za kisheria.
Mwisho
