USHIRIKIANO MPYA WA NM-AIST NA GLOBAL EDUCATION LINK KUFUNGUA FURSA ZA ELIMU NA UWEKEZAJI KWA VIJANA WENYE VIPAJI KUNUFAIKA

Geofrey Stephen
2 Min Read

Geofrey Stephen Arusha –

Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) imesaini hati ya makubaliano (MOU) na taasisi binafsi ya Global Education Link Ltd kwa lengo la kushirikiana katika nyanja za kitaaluma, uwekezaji na teknolojia.

Makubaliano hayo yamesainiwa Jumanne, Machi 10, 2026 katika makao makuu ya taasisi hiyo jijini Arusha. Hati hizo zilisainiwa na Makamu Mkuu wa NM-AIST, Profesa Maulilio Kipanyula, pamoja na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Global Education Link Ltd, Abdulmalik Mollel.

Habari Picha 9265
Akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini, Profesa Kipanyula alisema ushirikiano huo unatarajiwa kuongeza idadi ya wanafunzi wa kimataifa watakaokuja kusoma katika taasisi hiyo, pamoja na kuimarisha ubora wa elimu na tafiti za kisayansi.

Alieleza kuwa NM-AIST ilianzishwa kwa dhamira ya kuzalisha kizazi cha wanasayansi na wabunifu mahiri waliobobea katika sayansi, teknolojia na ubunifu. Lengo kuu ni kuwaandaa vijana watakaoweza kuleta mageuzi na mapinduzi ya kiuchumi katika jamii ya Tanzania.

Habari Picha 9251
Habari Picha 9250

Kwa upande wake, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Global Education Link Ltd, Abdulmalik Mollel, alisema taasisi yake imejipanga kikamilifu kuhakikisha makubaliano hayo yanatekelezwa ili kuongeza tija katika elimu na uwekezaji.

Mollel alisema uzoefu wake unaonyesha kuwa vyuo vikuu katika mataifa yaliyoendelea vinaunganisha elimu, uwekezaji na teknolojia kwa namna inayochochea maendeleo ya kiuchumi ya nchi zao.

Habari Picha 9258

“Tunashuhudia jinsi elimu inavyotumika kama chombo cha kutatua changamoto za kiuchumi kupitia maarifa wanayopata vijana katika vyuo vikuu,” alisema.

Aliongeza kuwa mataifa yaliyoendelea yamefanikiwa kwa sababu yaliwekeza katika vituo vya tafiti na teknolojia, jambo lililosaidia kubadilisha uchumi wa nchi zao.

Habari Picha 9256
Habari Picha 9257

“Kwa hakika, hakuna mabadiliko ya kweli ya kiuchumi yanayoweza kupatikana bila uwekezaji katika tafiti kutoka taasisi za elimu ya juu,” alisisitiza.

Habari Picha 9260
Habari Picha 9261

Ushirikiano huo unatarajiwa kufungua fursa mpya za elimu, tafiti na uwekezaji, huku ukiimarisha nafasi ya NM-AIST kama kituo muhimu cha maendeleo ya sayansi na teknolojia barani Afrika.

Habari Picha 9254
Habari Picha 9262

Mwishooo..

Share This Article
Leave a Comment